Urusi 2018: Nani atabeba Kombe? Tuimulike Uswisi
Ni hatua kwa hatua tunaendelea kuisogelea Juni 15 kushuhudia mtanange
wa kukata na shoka, Dar24 inaendelea kumulika timu moja baada ya
nyingine, leo tunaendelea na kundi E tukiigusa Uswisi.
Uswisi imeweka kwenye chungu cha kundi E pamoja na Brazil, Costa Rica na Serbia.
Timu ya Taifa ya Uswisi ilifuzu fainali za kombe la dunia 2018, ikitokea ukanda wa barani Ulaya (UEFA), ilipokuwa imepangwa katika kundi B (Kundi La Pili) lililokuwa na timu za Ureno, Hungary, Visiwa vya Faroe, Latvia na Andora.
Uswisi ilimaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi hilo kwa kufikisha alama 27, sawa na Ureno waliokuwa vinara, lakini walizidiwa kwa mabao ya kufunga na kufungwa, hivyo taifa hilo lenye watu zaidi ya 8,401,120, lililazimika kusubiri mchezo wa hatua ya mtoano ili kujihakikishia kucheza fainali za mwaka huu.
Mchezo wa mkondo wa kwanza kwa timu hizo ulichezwa Novemba 09, 2017 mjini Belfast katika uwanja wa Windsor Park, na Uswisi walifanikiwa kuwachapa wenyeji bao moja kwa sifuri lililofungwa na beki wa kushoto Ricardo Iván Rodríguez.
Mchezo wa mkondo wa pili ukachezwa Novemba 12, 2017 mjini Basel katika uwanja wa St Jacob Park na timu hizo zilitoka suluhu, na moja kwa moja wenyeji Uswizi walikata tiketi ya kucheza fainali za kombe la dunia.
Majina ya utani ya timu ya taifa ya Uswisi: Schweizer Nati (Swiss Nati), La Nati (The Nati), Rossocrociati (Swiss national team) na literally Red (Crusaders)
Mfumo: Kikosi cha Uswisi hutumia mfumo wa 4-5-1.
Mchezaji Nyota: Granit Xhaka (Arsenal)
Mchezaji hatari: Denis Zakaria (Borussia Mönchengladbach).
Nahodha: Stephan Lichtsteiner (Juventus)
Kocha: Vladimir Petković (54), raia wa Bosnian-Herzegovinian.
Ushiriki: Uswisi imeshiriki fainali za kombe la dunia mara tisa (9). Mwaka 1934, 1950, 1954, 1962, 1966, 1994, 2006, 2010 na 2014.
Mafanikio: Kufika Robo Fainali (1934, 1938 na 1954).
Kuelekea 2018:
Mashabiki wa soka nchini Uswisi tayari wameshajipa matumaini makubwa ya kuona timu yao ikifika mbali katika fainali za mwaka huu, na wengine wanatamba kupitia mitandao ya kijamii kwa kueleza watachukua ubingwa wa dunia katika ardhi ya Urusi.
Kocha Vladimir Petkovic ameeleza nia yake ya kutaka kuvunja rekodi ya kuivusha Uswisi katika hatua ya robo fainali, na na kisha kuongeza nguvu na kuiweka kileleni.
Kiungo Granit Xhaka anaaminiwa sana na kocha huyo katika mipango aliojipangia, kutokana na kuwa na msimu mzuri akiwa na klabu ya Arsenal ya Uingereza, japo klabu hiyo ilimaliza katika nafasi ya sita katika msimamo wa ligi.
Wachezaji wengine kama Xherdan Shaqiri (Stoke City) na Steven Zuber (Hoffenheim), Stephan Lichtsteiner (Juventus), Ricardo Rodríguez (AC Milan), Fabian Lukas Schär (Deportivo La Coruña) na chipukizi Manuel Obafemi Akanji (Borussia Dortmund), pia ni tegemeo kubwa kwa kocha huyo.
Kesho tutakuwa hapa tena kuimulika timu nyingine, hakikisha hauko mbali na Dar24 ili usiwe mbali na Urusi mwaka huu.
Uswisi imeweka kwenye chungu cha kundi E pamoja na Brazil, Costa Rica na Serbia.
Timu ya Taifa ya Uswisi ilifuzu fainali za kombe la dunia 2018, ikitokea ukanda wa barani Ulaya (UEFA), ilipokuwa imepangwa katika kundi B (Kundi La Pili) lililokuwa na timu za Ureno, Hungary, Visiwa vya Faroe, Latvia na Andora.
Uswisi ilimaliza katika nafasi ya pili kwenye kundi hilo kwa kufikisha alama 27, sawa na Ureno waliokuwa vinara, lakini walizidiwa kwa mabao ya kufunga na kufungwa, hivyo taifa hilo lenye watu zaidi ya 8,401,120, lililazimika kusubiri mchezo wa hatua ya mtoano ili kujihakikishia kucheza fainali za mwaka huu.
-
Urusi 2018: Nani atabeba Kombe? Tuimulike Brazil
Mchezo wa mkondo wa kwanza kwa timu hizo ulichezwa Novemba 09, 2017 mjini Belfast katika uwanja wa Windsor Park, na Uswisi walifanikiwa kuwachapa wenyeji bao moja kwa sifuri lililofungwa na beki wa kushoto Ricardo Iván Rodríguez.
Mchezo wa mkondo wa pili ukachezwa Novemba 12, 2017 mjini Basel katika uwanja wa St Jacob Park na timu hizo zilitoka suluhu, na moja kwa moja wenyeji Uswizi walikata tiketi ya kucheza fainali za kombe la dunia.
Majina ya utani ya timu ya taifa ya Uswisi: Schweizer Nati (Swiss Nati), La Nati (The Nati), Rossocrociati (Swiss national team) na literally Red (Crusaders)
Mfumo: Kikosi cha Uswisi hutumia mfumo wa 4-5-1.
Mchezaji Nyota: Granit Xhaka (Arsenal)
Mchezaji hatari: Denis Zakaria (Borussia Mönchengladbach).
Nahodha: Stephan Lichtsteiner (Juventus)
Kocha: Vladimir Petković (54), raia wa Bosnian-Herzegovinian.Mafanikio: Kufika Robo Fainali (1934, 1938 na 1954).
Kuelekea 2018:
Mashabiki wa soka nchini Uswisi tayari wameshajipa matumaini makubwa ya kuona timu yao ikifika mbali katika fainali za mwaka huu, na wengine wanatamba kupitia mitandao ya kijamii kwa kueleza watachukua ubingwa wa dunia katika ardhi ya Urusi.
Kocha Vladimir Petkovic ameeleza nia yake ya kutaka kuvunja rekodi ya kuivusha Uswisi katika hatua ya robo fainali, na na kisha kuongeza nguvu na kuiweka kileleni.
-
Urusi 2018: Nani atabeba Kombe? Tuimulike Nigeria
Kiungo Granit Xhaka anaaminiwa sana na kocha huyo katika mipango aliojipangia, kutokana na kuwa na msimu mzuri akiwa na klabu ya Arsenal ya Uingereza, japo klabu hiyo ilimaliza katika nafasi ya sita katika msimamo wa ligi.
Wachezaji wengine kama Xherdan Shaqiri (Stoke City) na Steven Zuber (Hoffenheim), Stephan Lichtsteiner (Juventus), Ricardo Rodríguez (AC Milan), Fabian Lukas Schär (Deportivo La Coruña) na chipukizi Manuel Obafemi Akanji (Borussia Dortmund), pia ni tegemeo kubwa kwa kocha huyo.
-
Urusi 2018: Nani atabeba Kombe? Tuimulike Croatia
Kesho tutakuwa hapa tena kuimulika timu nyingine, hakikisha hauko mbali na Dar24 ili usiwe mbali na Urusi mwaka huu.
0 Comments:
Post a Comment